
Mgombea Urais kutoka chama cha Liberal, Moon Jae-in ametaja kuwa angependa kuimarisha uhusiano na Korea Kaskazini.
Vyombo vya habari Korea Kaskazini vimesema kuwa vingependelea uongozi uliokuwa wa zamani ambapo mataifa hayo mawili yalikuwa ya kishirikiana na kuwasiliana.
Mgombea anayeegemea mrengo wa kushoto yuko kifua mbele huku yele mwenye msimamo wa kadri Ahn Cheol-soo akiwa mpinzani wake mkubwa.
Uchaguzi huo unaangaliwa wakati ambapo kuna tataizo la kiuchumi nchini humo na wasiwasi na Korea Kaskazini.
Bwana Moon anataka kuimarisha mawasiliano na Korea Kaskazini kinyume na aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo Park Geun Hye ambaye alikata uhusiano wote na taifa hilo.
Wachunguzi wanatarajia idadi kubwa ya watu kujitokeza huku idadi hiyo ikipigwa jeki na wapiga kura vijana huku Korea Kusini ikichagua rais kutoka kwa wagombea 13.
0 Post a Comment:
Post a Comment