Ukuta wawaua wageni 22 harusini India


11 Mei 2017

Ukuta ulioanguka na kuwaua wageni 22 harusini India


Ukuta ulioanguka
Haki miliki ya picha
Takriban watu 22 wamefariki baada ya ukuta kuwaangukia wakati wa harusi kaskazini mwa India.
Wageni hao walikuwa wamejikinga na mvua kubwa inayoendelea kunyesha kabla ya ukuta huo kuwaangukia.
Watu wengine 26 walijeruhiwa katika jali hiyo ya Bharatpur ,wilaya moja ya jimbo la Rajasthan ,15 kati yao wakiwa na majeraha mabaya.
Vyombo vya habari vinasema kuwa vibanda vya kuuza chakula vilikuwa vimewekwa kandakando ya ukuta huo karibu na harusi.
Ukuta huo na kibanda ulianguka kutokana na kimbunga kulingana na afisa wa Polisi Anil Tank aliyenukuliwa akisema.
Alisema kwamba ukuta huo wenye urefu wa futi 90 uliwaangukia wageni wengi.
''Waliojeruhiwa walikimbizwa katika hospitali za eneo hilo mara moja huku wakipewa matibabu''.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: