Korea Kaskazini yarusha kombora la kushambulia meli


 8 Juni 2017

Korea Kaskazini ikionyesha makombora ya Styx 2012
Korea Kaskazini ikionyesha makombora ya Styx 2012
Korea kaskazini imerusha makombora kadha ya kushambulia meli mashariki mwa pwani yake, kwa mujibu wa Korea Kusini
Mamlaka zilisema kwa makombora hayo yaliyorushwa Alhamisi asubuhi karibu na mji wa Wonsan yalikuwa ni ya masafa mafupi.
Makombora hayo yaliruka umbali wa kilomita 20o kabla ya kuanguka baharini.
Majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini mwaka huu yamekiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
Wataalamu wana hofu kuwa majaribio hayo na hatua za Korea kutundika silaha za nuklia katika vichwa vya makombora.
Msemaji wa Jeshi la Korea Kusini amesema kuw majiribio ya hivi punde yalionyesha kuwa Korea Kaskazini ilitaka kuonyesha kuwa ina uwezo wa kulenga meli kubwa baada ya mazoezi ya hivi majuzi kati ya Marekani na vikosi vya Korea Kusini.
Makomboa ya kushambulia meli ni makombora ambayo huelekezwa. Mwaka 2012 Korea Kaskazini ilionyesha makomboa kadha kama hayo yanayojulikana kama Styx.
Lakini hapo awali Korea ilijaribu bila mafanikio kufanyia majaribio makombora ya kushambulia meli.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: