Misaada ya chakula haiwafikii walengwa Nigeria



19 Juni 2017

Nigeria
Yemi Osinbajo mwenye kofia nyeusi akiwa pamoja na Kashim Shettima
Maofisa nchini Nigeria wamearifu kwamba nusu ya chakula cha msaada kilichokuwa kimepelekwa kwa watu waliosambaratishwa kutoka katika makaazi yao na kundi la wana mgambo wa kiislam hakijawafikia walengwa.Idadi ya watu hao inakadiriwa kufikia milioni tatu katika kipindi cha miaka nane ya uasi wa wapiganaji wa Boko Haram
Msemaji wa kaimu rais wa Nigeria, Yemi Osinbajo, amesema kwamba mfumo mpya umezinduliwa mapema mwezi huu, na kuleta mabadiliko makubwa katika usambazaji misaada ya kibinaadamu, huku dhana ya kuibwa kwa misaada hiyo na kwenda katika mikono isiyostahili ikirindima.
Kwa sasa, maelfu ya polisi na wanajeshi wamechukua hatua ya kusindikiza magari hayo yenye kusambaza misaada ya chakula, ili iweze kufika katika maeneo stahiki na kuwapa wenye uhitaji.
Zaidi ya magari ya misaada milioni moja yaliyosheheni nafaka yako njiani kuelekea Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo. Watu milioni moja unusu wako katika njaa kuu.
Nao wapiganaji wa Boko Haram wanaendelea na mashambulizi bila kukoma, pamoja na mashambulizi na wakati mgumu wanaokabiliana nao kutoka katika jeshi la Nigeria.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: