Wagombea wa Trump washinda uchaguzi Marekani

21 Juni 2017

Bi Karen Handel wa Democrat akifurahia ushindi wake
Bi Karen Handel wa Democrat akifurahia ushindi wake
Chama cha Republican kimeshinda uchaguzi muhimu wa bunge la Congress katika jimbo la Georgia ulioonekana na wengi kuwa kura ya maoni dhidi ya utawala wa rais Donald Trump.
Huku kura zote ikiwa zimehesabiwa, mgombea wa Republican Karen Handel alishinda kwa asilimia 53 huku mgombea wa Democrat akijipatia asilimia 47.
Katika Jimbo la Carolina Kusini, mgombea wa Republican Ralph Norman alimshinda mgombea wa Democrat Archie Parnell katika ngome ya wahafidhina.
Spika wa bunge Paul Ryan alimpongeza Bi Handel kwa ushindi huo mgumu.
Chama cha Democrat kilishindwa kwa kura chache katika maeneo ya Kansas na Montana mwaka huu.
Mgombea wa Republican Jon Ossoff baada ya ushindi wake

Mgombea wa Republican Jon Ossoff baada ya ushindi wake

Haki miliki ya pich

Katika jimbo la Georgia matumizi ya uchaguzi huo yalifikia dola milioni 56 ikiwa ndio uchaguzi uliogharamikiwa katika historia ya Marekani.
Bwana Ossoff alishindwa kupata asilimia 50 ya kura zilizohitajika ili kuibuka mshindi katika uchaguzi wa jimbo la Atlanta mnamo mwezi Aprili, hivyobasi kulazimisha awamu ya pili ya uchaguzi dhidi ya Handel.
Democrats walitumai kutumia fursa ya kushuka kwa umaarufu wa Trump kushinda kiti cha Georgia.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: