Aiba pesa pauni 100,000 benki kwa njia ya mtandao



21 Juni 2017
\Man holds a credit card while typing on a computer keyboard
Mdukuzi mmoja amefungwa jela baada ya kuiba karibu pauni 100,000 akitumia mfumo wa mtandao wa benki.
James Ejankowski, 24 aliibia benki ya Clydesdale and Yorkshire Banking Group zaidi ya pauni 99,000 mwezi Disemba mwaka 2016.
Kisha akatumia pesa hizo kununua magari aina ya BMW na Range Rover na pia akajichora chale usoni.
Alidanganya familia yake kuwa alikuwa ameshinda pesa hizo katika mchezo wa bahati nasibu.
Ejankowski aligundua kuwa ikiwa angetumia mfumo wa mtandao wa benki hiyo kuhamisha pesa kati ya akaunti zake usiku wa manane na saa saba asubuhi benki haingegundua.
Alitumia akaunti ya mpenzi wake Charlotte Slater kuhamisha pauni 53,399.
Licha ya kujinunulia vitu kadhaa Ejankowski, pia alitumia pesa zingine kulipa madeni yake na kampa shangazi yake puani 2000 na pauni 1,362 kwa baba mkwe.
Wiki nne baada ya kuanza kuiba, alijisalimisha kwa polisi na kukiri kuiba akisema kuwa alikuwa amebaki na pauni 40 tu.
Benki ya Clydesdale hata hivyo imefanikiwa kupata pauni 34,000.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: