Wanajeshi wa Ubelgiji wamemuua mlipuaji wa bomu mjini Brussels



21 Juni 2017

Polisi katika eneo la tukio
Polisi katika eneo la tukio
Wanajeshi wa Ubelgiji wamemuua kwa kumpiga risasi mlipuaji wa bomu wa kujitoa muhanga, katika kituo kikuu cha reli mjini Brussels.
Idara ya polisi imesema kuwa mtu huyo alikuwa amevalia kile kilichoonekana kuwa mkanda wa vilipuzi na kuwa kulitokea mlipuko mdogo.
Waendesha mashtaka wanasema kuwa mshukiwa huyo amefariki.
Watu waliokuwa katika kituo Kikuu cha mabasi mjini Brussels na eneo la karibu la mnara ambalo hufurika watalii wote waliondolewa.
Wanajeshi wamekuwa wakilinda doria mjini Brussels tangu mwaka uliopita kulipotokea shambulio la kujitoa mhanga katika eneo la Uwanja wa ndege na kwenye mfumo wa usafiri wa chini ya ardhi.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: