Wanasayansi wavumbua chanjo ya magonjwa ya moyo



20 Juni 2017

Netherland
Mfano wa chanjo hiyo
Shirika la utafiti wa kisayansi kutoka nchini Netherlands limeanza kufanya majaribio kwa wanadamu ya chanjo ya kupunguza kiwango cha mafuta katika mwili wa mwanaadamu na kwamba endapo utafiti huo utafanikiwa; wana matumaini kuwa chanjo hiyo itakuwa na uwezo wa kuzuia magonjwa ya moyo.
Watafiti hao wameeleza kuwa majaribio yao waliyokwisha kuyafanya dhidi ya panya yanaonesha kwamba chanjo hiyo imefanikiwa kuzuia na kuacha kuimarisha amana ya mafuta katika mishipa ya damu.
Imearifiwa kuwa chanjo hiyo ina uwezo wa kufanya mfumo wa kinga ya mwili kukabiliana na mafuta yasiyohitajika kutoka katika damu.
chanjo

WATU WENYE MIILI MIKUBWA KUWEZA KUUNGUZA MAFUTA
Wanasayansi hao wanaamini kuwa chanjo hiyo inaweza kutumika kama njia mbadala wa zilizokuwa za kupunguza mafuta , pamoja na kuwasaidia, mamilioni ya watu ulimwenguni kupambana na mafuta yasiyohitajika mwilini.
Inatarajiwa kuchukua takriban miaka sita ili vipimo hivyo kukamilika.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: