Trump: Uhusiano kati ya Marekani na Urusi umo hatarini

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

3 Agosti 2017

Trump and Putin at G20

Rais wa Marekani Donald Trump anasema kuwa uhusiano kati ya nchi yake na Urusi uko hatarini baada ya bunge la Congress kuiongezea Urusi vikwazo.
Bwana Trump alidhinisha hatua hiyo siku ya Jumatano.
Urusi nayo imesema kuwa vikwazo hivyo vipya ni kama kutangaza vita vya biashara dhidi ya Urusi.
Sheria hiyo inalenga kuiadhibu Urusi kwa madai ya kuingilia uchaguzi wa Marekani mwaka 2016 na vitendo vyake nchini Ukrain.
Trump alikuwa amepinga mswaada huo ambao unizichukulia hatua Iran na Korea Kaskazini, na unamzuia Trump kulegeza vikwazo hivyo bila idhini ya Congress.
Urusi imejibu kwa hasira vikwazo hivyo. Waziri mkuu Dmitry Medvedev alisema kuwa vikwazo vinamaliza matumaini ya kuboresha uhusiano kati ya Urusi na Marekani.
Kupitia ujumbe kwenye mtandao wa Facebook Medvedev aliandika kuwa hatua hizo zilionyesha udhaifu wa Trump.
Wiki iliyopita Urusi ilijibu kwa kuiamrisha Marekani kupunguza wanadiplomasia kwa watu 775.
Hatua hiyo inapunguza kiwango cha fedha ambazo Marekani itawekeza katika miradi ya nishati nchini Urusi na kufanya vigumu kwa kampuni za Marekani kufanya biashara na Urusi.
NIJUZE HABARI KWA 0625 966 236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: