Marubani wafukuzwa kazi baada ya kuruhusu mtoto kuendesha ndege

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

Marubani wafukuzwa kazi baada ya kuruhusu mtoto kuendesha ndege


Marubani wawili wanaofanya kazi na shirjka la ndege la serikali nchini Algeria wamefukuzwa kazi baada ya kumruhusu mtoto yatima mwenye umri wa miaka kumi kuendesha ndege ya abiria.
Mtandao wa Africa News unasema kuwa zoezi hilo liifadhiliwa na kurekodiwa na runinga ya El Bilad TV, waliomuonyesha mtoto huyo akiwa amavaa sare za rubani akibofya vitufe katika chumba cha rubani.
Haijulikani ni abiria wangapi walikuwa ndani ya ndege hiyo ya Air Algerie kutoka mji wa Algiers hadi mji Setif.
Mtandao huo unasema kuwa rubani hao walifukuzwa tarehe 29 mwezi Julai huku uchunguzi zaidi ukifanywa kwa sababu kitendo hicho kilikiuka sheria za usafiri wa ndege.
NIJUZE HABARI KWA 0625 966 236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: