Walinzi wa Trump kuifanyia majaribio ndege ya ulinzi

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

3 Agosti 2017

President Trump driving a golf buggy

Walinzi wa rais wa Marekani Donald Trump wana mipango ya kufanyia majaribio ndege ya ulinzi isiyo na rubani wakati Trump atazuru klabu yake ya gofu huko New Jersey baadaye mwezi huu.
Ndege ndogo itafanyiwa majaribio na walinzi wa rais katika uwanja wa Trump National Golf Club huko Bedminster
Trump anatarajiwa kufanya ziara ndefu katika klabu hiyo.
Walinzi wa rais wanasema kuwa watazifanyia majaribio ndege kadhaa zisizo na rubani kwa masuala ya ulinzi.
Wakati wa shughuli hii ndege hiyo itaruka umbali wa kati ya futi 300 na 400 au mita 91 na 121 angani.
Ndege hiyo ina kamera pande tofauti na walinzi wa Trumo wanasema watajulisha watu katika klabu kuwa ndege hiyo itakuwa ikihudumu eneo hilo.
Walinzi hao wanasema kuwa makao ya kibinafsi yanaweza kunaswa na kamera za ndege hiyo.
Picha na video ambazo zinatarekodiwa na ndege hiyo zitafutwa baada ya siku 30.
NIJUZE HABARI KWA 0625 966 236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: