ZANZIBAR: KITUO CHA MAFUTA CHAWAKA MOTO

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

17 Sep 2017


  Kituo cha United Petrolium kilichopo Kinazini mjini Unguja, kimeungua moto leo asubuhi baada ya mlipuko kutokea kwenye gari la kubebea mafuta la kampuni ya Bakhresa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Hassan Nassir Ali amesema chanzo cha tukio hilo lililotokea leo Jumapili saa 1:30 asubuhi ni gari la kampuni hiyo ambayo ndiyo mmiliki wa kituo hicho.
Amesema dereva wa gari hilo aliyetambuliwa kwa jina moja la Ismail alitoka ndani ya gari na kufunga mipira ili kuanza kushusha mafuta.
“Alipomaliza kufunga mipira kwenye visima vya mafuta, alipanda juu ya gari ili kuweka sawa mitambo lakini alipofungua mlango wa tangi lililopo juu ya gari ulitokea mlipuko uliosababisha moto mkubwa ulioenea kituoni na kwenye baadhi ya maduka yaliopo jirani na kituo,” amesema Kamanda Ali.
Amesema hasara iliyosababishwa na moto bado haijatambulika na kwamba, kikosi kazi kinaendelea kufanya tathmini.
Kamanda Ali amesema dereva ambaye alipata majeraha amepelekwa hospitalini kwa matibabu.
Amesema moto huo umezimwa na Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.
TUFUATE FACEBOOK. BONYEZA HAPA @ZAKACHEKA.HABARI

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: