Australia wapiga kura kwa wingi kuhalalisha ndoa za jinsia moja

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

Watu nchini Australia wamepiga kura kwa wingi katika hatua ya kuhalalisha ndoa za jinsia moja kwenye kura hiyo ya kihistoria.
Kura ilionyesha kuwa asilimia 61.6 ya watu walipiga kura kuruhuru wapenzi wa jinsi moja kufunga ndoa.
Wanaounga mkono ndoa za jinsia moja wamekuwa wakisherehekea maeneo ya umma wakiimba na kucheza,
Waziri mkuu Malcolm Turnbul alisema serikali yake kwa sasa itaruhusu kupitishwa sheria hizo bungeni ifikapo krismasi.
"Watu wa Australia wamezungumza kwa mamilioni na wamepiga kura kwa wingi kura ya ndio kuleta usawa wa ndoa, Bw Turnbull alisema baada ya matoko kutangazwa.


Haki miliki ya pichaGET
Image captionWatu wapiga kura kwa wingi kuunga mkono ndoa za jinsia moja Australia

Matokeo hayo ya Jumatano yanafikisha kikomo iliyokuwa wakati mmoja kampeni kali.
Kura hiyo yenyewe imekosolewa na wale wanaounga mkono ndo za jinsia moja wengine wakisema kuwa haikuhitajika wakati bunge lilikuwa na uwezo wa kuijadili moja kwa moja.
Wati walikuwa wanashiriki kwa hiari kinyume na uchaguzi ambao ni wa lazima nchini Australia.
Zaidi ya watu milioni 12.7 karibu asilimia 79.5 ambai ni wapiga kura walishiriki katika zoezi hilo la majuma 8 ambapo swali moja tu liliulizwa, "sheria ya ndoa inaweza kubadilishwa kuruhusu wapenzi wa jinsia moja kufunga ndoa.
Tuma habari, picha WhatsApp kwa 06259662
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: