Madaktari wanaogoma Uganda watoa masharti matatu

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM


Mulago
Rais wa chama cha madaktari nchini Uganda amewaambia waandishi wa habari nchini humo kwamba wako tayari kumaliza mgomo wao endapo mashariti yao matatu yatatekelezwa na serikali.
Miongoni mwa masharti hayo ni kulipwa marupurupu mbalimbali.
Daktari Ekwaru Obuku amesema kwamba wao wako tayari kurudi kazini iwapo serikali itazingatia masuala yao muhimu ikiwemo kuondoa kitengo maalum cha ungalizi wa afya kutoka ofisi ya Rais.
"Tunasema kabla ya turudi kazi, dawa zipo? Kabla ya turudi kazi, mshahara je? Na kitengo hiki wanaita kitengo cha uangalizi wa afya, wanawakamata na kuwaaibisha madaktari?" amesema Dkt Obuku.
Licha ya wananchi kutopata huduma za afya kutokana na mgomo huo na wao wametowa hisia zao:
"Serikali inatumia fedha nyingi kuwalipa wabunge milioni 30 mtu mmoja, ikiwa madaktari wanaambiwa hakuna fedha ni jambo la kusikitisha," amesema mmoja wa wakazi.
"Kwa maoni yangu serikali inatakiwa kuwalipa vizuri madaktari na walimu ni watu muhimu katika taifa."
Raia mwingine Peter Kwizera Ronald alisema ni jambo la kusikitisha kwamba pesa za madaktari hazipatikani ilhali wabunge wanalipwa pesa nyingi.

Tuma habari picha WhatsApp kwa 0625966236

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: