Zimbabwe:Mnangagwa aanza kuchapa kazi

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>

Rais mpya wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ametangaza msamaha wa miezi mitatu kwa watu binafsi na kampuni mbalimbali ambazo zimeficha fedha za umma kinyume cha sheria nje ya nchi hiyo kuzisalimisha.
Kupitia taarifa, amesema kwamba serikali itawakamata na kuwafungulia mashtaka wale watakaokataa kufanya hivyo kabla ya msamaha huo kumalizika Februari.
"Vitendo kama hivi ni uhalifu wa hali ya juu wa kiuchumi dhidi ya watu wa Zimbabwe," Bw Mnangagwa amesema.
Tangu aapishwe Ijumaa wiki iliyopita, Mnangagwa ameahidi kukabiliana na rushwa.
"Fedha nyingi na mali ya umma vimefichwa nje ya nchi na watu binafsi na mashirika," amesema.
"Wale waliohusika wanahamasishwa kutumia fursa hii a miezi mitatu kurejesha fedha hizo na mali ili kuepuka uchungu na aibu ya kutembelewa na mkono mrefu wa sheria," ameongeza.
Mtangulizi wake, Robert Mugabe, aliondoka madarakani wiki iliyopita baada ya jeshi kuingilia kati.
Alikuwa ameongoza nchi hiyo kwa miaka 37 tangu uhuru.

Tuma habari picha, video za matukio mbalimbali WhatsApp kwa 0625966236

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: