Wanajeshi wa DR Congo wauliwa na wenzao wa Rwanda

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>
Wanajeshi watano wa DR Congo wameuawa na wanajeshi wa Rwanda kulingana na jeshi la nchi hiyo
Jenerali Bruno Mandevu alisema kuwa vita vilizuku katika mbuga ya wanyama ya Virunga katika ardhi ya Congo , madai ambayo Rwanda imekana.
Amesema kuwa wanajeshi wa Congo walidhania kwamba walikuwa wakikabiliana na waasi waliopo katika eneo hilo.
Wengine wanahofia kwamba mapigano huenda yakaongeza hali ya wasiwasi iliopo kati ya mataifa hayo mawili ambayo yana historia mbaya.
Rwanda iliwavamia mara mbili majirani zake 1990.
Msemaji wa jeshi la Rwanda kanali Innocent Munyengango alithibitisha kutokea kwa mashambuliano hayo na kusema hakukuwa na majeraha upande wa Rwanda.
''Jeshi la Congoleese lilivamia kambi yetu na kutushambulia. Wanajeshi wetu walilazimika kujitetea'', alisema.
Mashariki mwa taifa la DR Congo karibu na mpaka na Rwanda ni eneo ambalo limekuwa halina udhibiti.
Mbuga ya wanyama pori ya Virunga DR Congo
Image captionMbuga ya wanyama pori ya Virunga DR Congo
Mashirika ya misaada yanaonya kutokea kwa ghasia katika mkoa wa Ituri uliopo Kaskazini mashariki, ambapo UNICEF inasema zaidi ya watoto 46,000 wametoroka.
Vijiji vilivyochomwa katika mkoa huo ambapo watu kutoka makundi ya Hema na Lendu wamekuwa wakipigania udhibiti.
Mapema wiki hii, Baraza la wakimbizi nchini Norway limeonya kwamba mzozo nchini DR Congo unakaribua kutibuka.
Katika kipindi cha miaka miwili iliopita, watu zaidi wamewachwa bila makao nchini DR Congo zaidi ya nchi nyengine yoyote. Jumla ya watu milioni 4.5 wanaihitaji msaada
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: