Japan yaishutumu Korea Kaskazini kwa kurusha makombora


29 Mei 2017

Shinzo Abe amesema anaiheshimu Korea Kaskazini
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe ameishutumu Korea Kaskazini kutokana na majaribio yake ya makombora katika bahari nchini Japan.
Amesema kuwa hata katika mkutano wa G-7 wa hivi karibuni chokochoko za Korea Kaskazini zilijadiliwa kwa uzito mkubwa.
Waziri Abe amesema kuwa Japan itashirikiana na mataifa mengine ikiwemo Marekani kukabiliana na vitisho vya Korea Kaskazini.
Ameahidi kuunga mkono makubaliano ya mkutano wa G-7.
Waziri kiranja nchini Japan Yoshihide Suga, anasema kuwa majaribio haya ya makombora ya Korea Kaskazini yanahatarisha shughuli za uchukuzi ndani ya Bahari nchini Japan.
Katika siku za hivi karibuni Korea Kaskazini imekuwa na choko choko dhidi ya Marekani kuhusiana na mpango wake wa nyuklia na hatimaye Japan nayo imeguswa na harakati hizo za Korea Kaskazini.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: