Korea Kaskazini: Tuko tayari kuzungumza na rais Trump


13 Mei 2017

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Korea Kaskazini imesema kuwa itafanya mazungumzo na Marekani iwapo mazigira yataruhusu ,kulingana na vyombo vya habari vya Korea Kusini.
Mjumbe mwandamizi wa Korea Kaskazini amesema kuwa mazungumzo na serikali ya rais Trump yanawezekana kufuatia mkutano na waliokuwa maafisa wa serikali ya Marekani nchini Norway.
Awali mwezi huu rais wa Marekani Donald Trump alisema itakuwa heshima kubwa kukutana na rais Kim Jong un.
Matamshi yake yanajiri kufuatia ongezeko la hali ya wasiwasi kuhusu mipango ya Korea Kaskazini ya kinyuklia pamoja na ile ya utengezaji wa makombora ya masafa marefu.
Choe Son Hui ambaye ni afisa katika wizara ya maswala ya kigeni kuhusu maswala ya Marekani kaskazini alitoa matamshi hayo wakati alipokuwa akirudi Pyongyang baada ya mkutano mjini Oslo.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: