Waasi wa Sudan wakiri kuhusika na shambulio la mabasi huko Somalia



9 Juni 2017

Waasi wa Sudan Kusini
Waasi wa Sudan Kusini



Waasi wa Sudan Kusini wamesema walihusika katika shambulio la msafara wa mabasi yaliokuwa yakielekea Juba lililosababisha vifo vya watu 14.
Msemaji wao ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba kikosi hicho cha waasi kilikuwa kinalenga kikosi cha serikali.
Lam Paul Gabriel aliongeza kwamba wanajeshi hao walikuwa wanawasindikiza raia na waliuawa katika kisa cha ufyatulianaji wa risasi.
Bwana Lam amesema wapiganaji wake waliwaua watu 40 , ikiwemo makanali wawili katika shambulio lililo tumia roketi ya propela ya Gruneti.
Lakini Msemaji wa polisi wa Sudan Kusini , Daniel Justin Boulogne, amesema ni watu 14 waliouawa.
Radio ya Sudan Kusini ya Eye imechapisha kwenye mtandao wake wa Tweeter kuhusiana na idadi kamili ya watu waliouawa.


Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: