Wanafunzi wavamia na kuwapiga walimu Kenya



20 Juni 2017

Wanafunzi wawatandika walimu Kenya
Shule moja nchini Kenya imefungwa baada ya wanafunzi kuwavamia na kuwapiga walimu, kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la nchi hiyo.
Gazeti hilo linasema kuwa wanafunzi hao walionekana wakiwa na rungu na viboko wakiwavamia walimu wa kike ambapo walimu watatu walipata majeraha mabaya.
Baadaye polisi walifika katika shule ya msingi ya Kirimon na kufyatua risasi hewani.
Televisheni ya NTV nchini Kenya, ilisema kuwa wanafunzi walikuwa wakilalamikia adhabu ambayo walipewa.
Waakilishi kutoka chama cha walimu walisema shule hiyo itafungwa hadi Ijumaa wakati mkutano kati ya walimu, wazazi na wizara ya elimu utafanyika.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: