Mbunge wa Chadema akamatwa

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

2 Agosti 2017


Mbunge wa Jimbo la Mbozi Mkoani Songwe, Pascal Haonga, amekamatwa na Polisi mchana huu katika mji mdogo wa Mlowo-Mbozi.
Mbunge huyo anahojiwa na polisi na sababu za kukamatwa kwake bado hazijafahamika.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Mathias Nyange, amethibitisha kumshikilia Haonga lakini hakutaka kueleza suala hilo kwa kina kwa madai yupo nje ya ofisi.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Songwe, Meshack Mgaya amesema wanaendelea kufuatilia kwa ukaribu juu ya tukio hilo na baadae chama kitatoa tamko baada ya kujiridhisha sababu za kukamatwa kwa Mbunge huyo.
NIJUZE HABARI KWA 0625 966 236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: