Rais Trump aidhinisha vikwazo dhidi ya Urusi

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

2 Agosti 2017

Trump and Putin at G20
Rais wa Marekani Donald Trump ameusaini kuwa sheria mswada ambao utaiwekea vikwazo vipya Urusi, kwa kuingilia kati uchaguzi wa Marekani mwaka 2016.
Mswada huo ambao uliwekwa sahihi kisiri katika Ikulu ya White House pia inaziwekwa viwazo Iran na Korea Kaskazini.
Sheria hiyo inamzuia Trump kutokana na kuipunguzia vikwazo Urusi bila ya idhini ya bunge la Congress.
Urusi inakana kuingilia uchaguzi wa Marekani naye Trump akikana kushirikiana na Urusi.
Trump aliishutumu Congress ambayo wiki iliyopita ilipitisha kwa wingi mswaada huo na kuutuma kwenda Ikulu
Urusi tayari imejibu kwa kuwaamrisha wanadiplomasia 755 kuondoka kutoka ofisi zake za kibalozi.
Vikwazo hivyo vinakuja miezi kadhaa baada ta Rais Obama kuwatimua wanadiplomasia 35 wa Urusi.
Seneta wa Republican Lindsey Graham aliupongeza mswaada huo wakati ulipita.
"Rais Putin alifanya kitu ambacho hakuna yeyote nchini Marekani anaweza kukifanuya. aliileta pamoja Congress" alisena Graham.
NIJUZE HABARI KWA 0625 966 236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: