KUWAIT YAMFUKUZA BALOZI WA KOREA KASKAZINI

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

17 Sep 2017Kuwait yamfukuza balozi wa Korea Kaskazini
Ripoti kutoka nchini Kuwait zinasema kuwa imemfukuza balozi wa Korea Kaskazini.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa lakini kuwait imewaambia waandishi wa habari kuwa balozi wa Korea Kaskazini, amepewa mwezi mmoja kuondoka huku wanadiplomaisa wa Korea Kaskazini wakipunguzwa.
Kuwait ndiyo nchi pekee katika ghuba iliyo na ubalozi wa Korea Kaskazini.
Maelfu ya raia wa Korea Kaskazini wanafanya kazi nchini kuwait na nchi zingine za ghuba kama vibarua.
Hatua hiyo inachukuliwa wiki mbili baada ya kiongozi wa kuwait kuzuru Washington.
Marekani imetaka hatua za kimataifa kuchukuliwa dhidi ya Korea Kaskazini kufuatia mipango yake ya nyuklia.

TUFUATE FACEBOOK: @ZAKACHEKA.HABARI

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: