MTESIGWA AACHIWA BAADA YA KUKAMATWA NA POLISI

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

25 Sep 2017

Peter Msigwa

Mbunge wa Iringa Peter Msigwa


Polisi mjini Iringa imemuachia mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa kwa sharti la kumtaka arudi polisi Jumatatu.

Taarifa zinasema mbunge huyo ambae pia ni mchungaji wa kanisa alikamatwa pindi alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika eneo la Mlandege huko Mkoani Iringa.
Kwa mujibu wa msemaji wa Chadema Tumaini Makene, polisi inadai kumkatama Msigwa kwa tuhuma za uchochezi.
Msingwa anatoka chama cha Chadema ambacho ndio chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na kamata kamata ya wabunge nchini Tanzania kutoka upinzani hasa Chadema.
Miongoni mwa waliokumbwa na kamata hiyo hivi karibuni ni mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambae hivi sasa yuko nchini Kenya kwa ajili ya matibabu baada ya kupigwa risasi na watu ambao mpaka sasa hawajafahamika huko Dodoma, bungeni.
Zachary B. John 0625 966 236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: