WAISRAELI WATATU WAUAWA NA MPALESTINA KWA RISASI

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

26 Sep 2017Scene of attack at Har Adar (26/09/17)Watu watatu raia wa Israel wameuawa kwa kupigwa risasi na raia wa Palestina katika mlango wa kuingia kwenye makao ya walowezi wa kiyahudi eneo la Har Adara lililo ukingo wa magharibi.
Mtu mwenye bunduki wa umri wa miaka 37 kutoka kijiji kilicho karibu pia alipigwa risasi na kufariki baadaye.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema mauaji hayo yamesababishwa na uchochezi upande wa palestina.
Mauaji hayo yanafanyika wakati mjumbe wa Rais Donald Trump eneo la Mashariki ya Kati Jason Greenblat, anapowasili Jerusalem kufufua mazungumzo kati ya Israeli na Palestina.
Ikulu ya Marekani inasema kuwa imejaribu kufanya mikakati wa kuyafufua mazungumzo tangu Donald Trump aingie madarakani mwezi Januari lakini hakujakuwa na dalili za kuwepo hatua.
Mazungumzo ya amani kati ya pade hizo mbili yalivunjika mwezi Aprili mwaka 2014.
Polisi wanasema kuwa mtu huyo mwenye silaha anayetajwa na vyombo vya habari nchini Israeli kama Nimer Jamal, alishambulia baada ya kugundua kuwa alishukiwa na walinzi karibu na mlango wa eneo la Har Adar.
Aliwapiga risasi walinzi wawili na polisi wa mpaka kwa karibu, na kumjeruhi vibaya mtu mwingine kabla ya kupigwa risasi na vikosi vya usalama.
Haki miliki ya picha
Alitoka kijiji cha Beit Surik, karibu maili moja mashariki mwa Har Adar.
Eneo hilo liko karibu kilomita 18 kaskazini magharibi mwa Jurusalem.
Karibu Wapalestina 36,000 wana vibali vya kufanya kazi katika makao ya wayahudi ambapo ulinzi wa kuyalinda dhdi ya mashambulizi ni mkali.
Zaidi ya wayahudi 600,000 wanaishi karibu makao 140 yaliyojengwa tangu mwaka 1967, kwenye ukingo wa magharibi na Mashariki mwa Jerusalem.
TUFUATE FACEBOOK:ZAKACHEKA.HABARI

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: