UCHAGUZI KENYA: MKUU WA TUME YA UCHAGUZI AKUTANA NA RAILA ODINGA

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM
19 Oktoba 2017
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya Wafula Chebukati akutana na mgombea urais wa upinzani Raila Odinga.
Bw Chebukati amesema anatarajia kukutana na mgombea wa chama tawala cha Jubilee Uhuru Kenyatta baadaye.
"Mkutano huo utafuatwa na mkutano wa pamoja wa wawili hao," ameandika kwenye Twitter.
Gazeti la kibinafsi la Nation limesema wawili hao walikutana kwa takriban dakika 40 katika makao makuu ya tume hiyo Nairobi.
Mwenyekiti huyo alikuwa awali ameitisha mkutano wa wagombea urais wote leo adhuhuri lakini akauahirisha mapema leo asubuhi.
Uchaguzi mpya umepangiwa kufanyika Alhamisi wiki ijayo.
Hata hivyo, ingawa Rais Uhuru Kenyatta amesisitiza yuko tayari kwa uchaguzi huo na utaendelea, mgombea wa upinzani Raila Odinga alijiondoa wiki iliyopita.
Jana, Bw Odinga, ambaye ni mgombea wa muungano wa National Super Alliance (Nasa) alitangaza kwamba siku hiyo badala ya kushiriki uchaguzi, wafuasi wake watafanya maandamano makubwa kote nchini.
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati siku ya Jumatano alikuwa amewalaumu wanasiasa wa kusababisha kuwepo kwa mazingira yanayoifanya vigumu kuandaa uchaguzi huru na wa haki.
Alisema alikuwa anawapa "kadi ya manjano".
Waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang'i tayari ametangaza Alhamisi kuwa siku ya mapumziko.
FACEBOOK: zakacheka.blogspot.com na downloa App yetu huko.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: