Michael Flynn akiri kuwahadaa FBI

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>
Aliyekuwa mshauri mkuu wa masuala ya usalama wa taifa wa Donald Trump, Michael Flynn, amekiri kwamba aliandikisha taarifa ya uongo kwa idara ya uchunguzi wa jinai ya Marekani, FBI, mwezi Januari.
Bw Flynn alishurutishwa kujiuzulu mwezi mmoja baada yake kupotosha ikulu ya White House kuhusu mkutano wake na balozi wa Urusi kabla ya Trump kuingia madarakani.
Mashtaka dhidi yake yaliwasilishwa na mwanasheria maalum Robert Mueller kama sehemu ya uchunguzi kuhusu tuhuma kwamba Urusi iliingilia uchaguzi wa Marekani wa 2016.
Bw Flynn alifika mahakamani Ijumaa.
Alikiri kosa moja ya kutoa makusudi "taarifa za uongo, za kubuni na za kupotosha".
Kwa mujibu wa mwanahabari wa AFP, Bw Flynn aliulizwa na Jaji Rudolph Contreras iwapo alitaka kukiri makosa hayo na akajibu kwa kusema "Ndio".
Jaji aliendelea: "Nakubali kukiri kwako makosa. Hivyo hakutakuwa na kusikizwa kwa kesi na labda huenda kusiwe na rufaa."
Alijisalimisha kwa FBI kabla ya kufanyika kwa kikao cha mahakama Ijumaa asubuhi mjini Washington DC.
Msaidizi huyo wa zamani wa Trump ndiye afisa wa ngazi ya juu zaidi katika utawala wa Trumpa ambaye amepatikana na hatia katika uchunguzi huo unaoendeshwa na Mueller.

Oktoba, meneja wa zamani wa kampeni za urais wa Trump, Paul Manafort, alituhumiwa kula njama ya kuilaghai Marekani katika shughuli za kibiashara na Ukraine.
Aidha, iliibuka kwamba msaidizi mwingine wa zamani, George Papadopoulos, amekiri makosa ya kutoa taarifa za uongo kwa maajenti wa FBI.

Tuma habari picha, video za matukio mbalimbali WhatsApp kwa 0625966236


Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: