Ajali ya gari Kenya 24 wapoteza maisha




Ajali hiyo iliyohusisha basi la kubeba abiria na lori la kusafirisha mafuta ghafi ya kupikia ilitokea katika eneo la Kiambu, karibu na Mtito Andei.
Mkuu wa polisi wa eneo la Kibwezi Leonard Kimaiyo ameambia BBC kuwa watu 23 walifariki papo hapo na mwingine mmoja alifariki alipokuwa akipata matibabu.
Watu 20 walipata majeraha na kupelekwa katika hospitali za miji ya Kibwezi na Makindu.
 Kimaiyo amesema walionusurika waliwaambia maofisa wa polisi kuwa dereva wa basi alikuwa akijaribu kupita gari jingine na kusababisha basi hilo kugongana na lori hilo.
Kwa mujibu wa Mamlaka ya Taifa ya Uchukuzi Kenya, watu 3,000 hufariki kila mwaka kutokana na ajali za barabarani.



                         comment, like and share
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: