Dk Magufuli ateua kamati ya pili kuchunguza mchanga wa madini

Dk Magufuli ateua kamati ya pili kuchunguza mchanga wa madini

   


Rais John Magufuli
Rais John Magufuli 
Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameteua wajumbe nane wa kamati maalum ya pili itakayofanya uchunguzi wa madini yaliyomo kwenye mchanga wenye madini ulio ndani ya makontena yaliyopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Taarifa iliyotolewa leo asubuhi na  Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imewataja wajumbe hao kuwa ni Profesa Nehemiah Osoro, Profesa Longinus Rutasitara, Dk Oswald Mashindano na Gabriel Malata.
Wengine ni Casmir Kyuki, Butamo Philip, Usaje Usibwe na Andrew Massawe.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa wajumbe hao wataapishwa kesho Aprili 11 saa 3:00 asubuhi Ikulu jijini Dar es Salaam.
 
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: