Watumwa wa jamii ya Yazidi waokolewa Iraq


  • 1 Mei 2017
Wayazidi 36 walipelekwa Dohuk Kaskazini mwa Iraq
 Wayazidi 36 walipelekwa Dohuk Kaskazini mwa Iraq
Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Iraq, inasema kuwa watu 36 wa kabila la Yazidi, waliotekwa kama watumwa na kundi la Islamic State, wameokolewa wakiwemo wanawake na watoto.
Wanaripotiwa kuwa kizuizini kwa karibu miaka mitatu.
Islamic State iliwauwa na kuwateka watu wengi wa Yazidi, ambao ni wa dini tofauti, wakati IS iliteka eneo la kaskazini mwa Iraq, mwaka 2014.
Wakurdi wa Peshmerga walidhibiti eneo hilo mwaka 2015 lakini Wayazidi wengi walikiliwa na Islamic State maeneo mengine wakati kundi hilo lilidhibiti sehemu kubwa za Kaskazini mwa Iraq.
Watu hao 36 walifika mji wa Dobuk siku mbili zilizopita ambapo walipewa hifadhi kwenye vituo vya Umoja wa Mataifa
Wanajumuishwa na familia zao huko na kupewa mahitaji ikiwemo nguo na madawa pamoja na ushauri wa kisaikolojia.
Umoja wa mataifa unaamini kuwa hadi wanawake na wasichana 1500 bado wanashikiliwa na huenda wanakumbwa na dhuluma za kingono.
 Mshirikishe Mwenzako: zakacheka.blogspot.com/ www.zakacheka.simplesite.com +255 625966236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: