Je, kila anayejiita nabii anayanena yaliyo ya Mungu?

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>

Kuelekeza waumini kula nyasi, kuwapulizia dawa za kuua wadudu machoni waumini kwa ahadi ya kupata utajiri, kupata uponyaji na kuuona ufalme wa Mungu ni miongoni mwa yale ambayo wamekuwa wakihubiri wale wanaojiita manabii ama watumishi wa Mungu barani Afrika.
Katika tukio la hivi karibuni nchini Tanzania Jeshi la polisi nchini humo linamshikilia mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Onsemo Machibya maarufu kwa jina alilojipa la Nabii Tito.
Mhubiri huyo anadaiwa kusambaza dini yake kupitia vipeperushi na picha za video, huku maudhui ya imani hiyo yakidaiwa kukinzana na maadili ya Kitanzania.
Jeshi la Polisi katika taarifa yake kwa vyombo vya habari lilisema mwanamume huyo ana matatizo ya akili na bado linaendelea kumshikilia.
Tito alijizolea umaarufu mitandaoni siku za hivi karibuni baada ya kusambaa kwa video zake kadhaa zikimuonyesha yeye na walioelezwa kuwa ni waumini wake wakinywa pombe wakati wa ibada yao lakini pia kucheza nyimbo mbalimbali hasa kwa kunengua viuno.
Kwenye moja ya video hizo, anaonekana kumbusu mdomoni aliyedaiwa kuwa mkewe pamoja na mwanamke mwingine anayedaiwa kuwa kijakazi wake.
Nabii Tito kwenye video hiyo anasema maandiko yameruhusu mwanaume kufanya zinaa na kijakazi wake.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: