Clinton: Nalaumu FBI na wadukuzi wa Urusi


  • 3 Mei 2017
Hillary Clinton amelilamu shirika la FBI na wadukuzi wa Urusi kwa kushindwa kwake katika uchaguzi mkuu
Hillary Clinton amelilamu shirika la FBI na wadukuzi wa Urusi kwa kushindwa kwake katika uchaguzi mkuu
Aliyekuwa mgombea wa urais nchini Marekani Hillary Clinton amewalaumu wadukuzi wa Urusi na mkurugenzi wa Ujasusi nchini humo kwa kushindwa kwake katika uchaguzi mkuu uliopita
Aliambia mkutano mjini New York kwamba angeshinda kura hiyo iwapo uchaguzi huo ungefanyika tarehe 20 mwezi Oktoba kabla ya kuchapishwa kwa barua ya mkurugenzi wa FBI James Comey akilielezea bunge la seneti kwamba FBI imeanzisha uchunguzi kuhusu hatua yake ya kutumia barua pepe za binafsi.
Alisema kwamba alikuwa amefanya kampeni nzuri na akapoteza kutoka na maswala yaliofanyika katika kipindi cha siku kumi za mwisho.
Anasema kuwa sasa amerudia uanaharakati akisema hatua yake inalenga kuweka upinzani mkali dhidi ya rais Trump ambaye amemkosoa kwa sera zake za kigeni mbali na utumizi wake wa mtandao wa Twitter.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: